“RAIS DKT.SAMIA ANAFANYA KILA JITIHADA KUWALIPA WAKANDARASI WAZAWA,” ULEGA
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega, amewatoa hofu wakazi wa Buyagu Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza na kuwataka wawe wavumilivu kwani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anafanya kila jitihada kuhakikisha anawalipa wakandarasi wa ndani ili kazi za ujenzi wa maegesho ya vivuko na miundombinu yake ikiwemo majengo ya kupumzikia abiria, vyoo, ujenzi wa kivuko kipya kitakachotoa huduma kati ya Buyagu na Mbalika pamoja na barabara ambayo itakuwa ikielekea eneo kivuko kinaposinama kushusha abiria ziweze kufanyika na kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma stahiki.