Ujumbe wa Mtendaji Mkuu

Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania TEMESA ni Wakala wa Serikali chini ya Wizara ya Ujenzi ulioanzishwa ili kutoa huduma za matengenezo ya Magari ya Serikali, Ushauri wa kihandisi katika fani za Umeme na Elektroniki, Ukodishaji Mitambo, Usimamizi wa Vipando pamoja na Uendeshaji na usimamizi wa Vivuko hapa nchini.



Ni heshima kubwa kwangu kuwaalika wadau wetu wote, taasisi za Serikali, Sekta binafsi na wananchi kwa ujumla kuendelea kushirikiana nasi katika kupata huduma. TEMESA imejizatiti kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu, zinazoendana na maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya sasa ya wateja.



Tunaelewa umuhimu wa huduma zetu katika kuimarisha ufanisi wa taasisi na kuchangia maendeleo ya uchumi wa Taifa. Hivyo, tumejipanga kuhakikisha tunatoa huduma bora, salama, za kuaminika, kwa wakati na kwa viwango vinavyokidhi matarajio ya wateja wetu.



Kupitia uwekezaji katika teknolojia za kisasa, uboreshaji wa mifumo ya utoaji huduma, pamoja na kuendeleza wataalamu wetu, tunaendelea kuongeza ubora na kasi ya huduma zetu kila siku. Aidha, tunazingatia uwajibikaji, maadili ya kazi na huduma kwa mteja kama msingi wa mafanikio yetu.



Ninawakaribisha sana kushirikiana nasi na kujionea ubora wa huduma za TEMESA. Tupo tayari kuwahudumia kwa weledi na ufanisi unaostahili.
Karibuni sana TEMESA, "Huduma Bora kwa Fursa za Maendeleo"


Kheri A. Mahimbali

Mtendaji Mkuu