Mkurugenzi wa Idara ya Matengenezo na Huduma za Ufundi

Mkurugenzi atafanya kazi zifuatazo;


(i) Kusimamia majukumu ya matengenezo ya magari ya serikali, mitambo na vifaa, huduma za umeme na elektroniki kwa kuunda programu fupi na ndefu za kazi na kusimamia utekelezaji wake.


(ii) Kusimamia ushauri wa kiufundi na huduma za ushauri kwa kuunda programu fupi na ndefu za kazi na kusimamia utekelezaji wake.


(iii) Kuunda mifumo bora ya matengenezo na usimamizi wa ukodishaji mitambo.

(iv) Kushauri juu ya maendeleo na usasishaji wa kazi za matengenezo na hati za kukodisha vifaa, miongozo na viwango.


(v) Kuunda na kusimamia mipango madhubuti ya kuimarisha karakana za Wakala.

(vi) Kutengeneza programu za kuwajengea uwezo ili kuimarisha uwezo wa kufanya kazi kwa matengenezo na huduma za ushauri ili kufikia viwango vya huduma bora vya kimataifa.


(vii) Kuanzisha na kusimamia utekelezaji wa matengenezo na viwango vya ubora wa ushauri kwa huduma za kazi za umeme, mitambo na elektroniki.


(viii) Kuanzisha na kukuza sera na mipango itakayoongeza ubora wa umeme.

(xi) Kuandaa programu bora za huduma za kukodisha mitambo ili kuhakikisha kuwa TEMESA inakuwa chanzo cha kuaminika cha huduma za kukodisha mitambo.

(x) Kuendeleza na kutekeleza uwezo wa kitaalam katika kazi za matengenezo na huduma za ushauri.