MUHTASARI WA HOTUBA YA MAKADIRIO YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

Imewekwa Wednesday 29th May , 2024

MUHTASARI WA HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI MHESHIMIWA INNOCENT LUGHA BASHUNGWA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

  • A.UTANGULIZI
  • 1.Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja kwamba, kufuatia taarifa iliyowasilishwahapaBungeninaKamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, iliyochambua utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Ujenzi ya mwakawa fedha 2023/24,Bungelako Tukufu sasalikubali kupokea na kujadili Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ujenzi, kwa mwaka wa fedha 2023/24. Ninaliomba Bunge lako Tukufu liridhie kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Ujenzi, kwa mwaka wa fedha 2024/25.
  • 2.Mheshimiwa Spika, awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kusimama leo hii mbele ya Bunge lako Tukufu. Naomba Hotuba yangu yote iingie katika kumbukumbu za Bunge kama ilivyowekwa mezani.

  • 3.Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanzakusimamambeleyaBungelako kuwasilisha Hotuba nikiwa Waziri wa Ujenzi, nitumie fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Samia SuluhuHassan,RaiswaJamhuriyaMuungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, kwa kuendelea kuniamini na kuniteua kuwa Waziri wa Ujenzi tangu tarehe 30 Agosti, 2023. NinamuahidiMheshimiwaRaiskuwakupitia dhamana hii aliyonipa, nitafanya kazi kwa weledi, bidii, uaminifunaubunifukwakushirikianana watumishi wenzangu katika Wizara na wadau wa Sekta ya Ujenzi, ili kuhakikisha kuwa sekta hii inakua na kuendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini. Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassanni Kapteni wajahazimakini,jasiri,mtulivu,mchamungu, mnyenyekevu Chifu Hangaya; ambaye ameongoza nchi yetu kupita mawimbi makali na magumu. Pale Nchi yetu ilipoondokewa na mpendwa wetu hayati Dkt. John Pombe Magufuli(RIP), Rais Samia alituvusha salama katika kipindi hicho cha majonzi na kigumu, alituvusha katika kipindi cha COVID na milipuko ya magonjwa duniani; ametuvusha salama hata kwenye mvua za El Nino na kimbunga Hidaya kwa fedha za dharura, na ameendelea kuiheshimisha nchi yetu katika nyanja za kimataifa na kidiplomasia. Hongera sana Chifu Hangaya, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

  • 4.Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuwapongeza Mheshimiwa Dkt. Philip Isdory Mpango, Makamu wa Rais; Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu, na Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, kwa namna ambavyo wanamsaidia Mheshimiwa Rais katika majukumu ya kuitumikia nchi yetu. Nawashukuru pia viongozi hawa kwa miongozo na maelekezo mbalimbali wanayonipatia katika kuisimamia Wizara ya Ujenzi. Ninawashukuru pia Mawaziri wenzangu na Naibu Mawaziri wote kwa ushirikiano wanaonipatia katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara.
  • 5.Mheshimiwa Spika, ninaishukuru Kamatiya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, chini ya uongozi wa Mwenyekiti, Mheshimiwa Selemani Kakoso (Mb. Mpanda Vijijini) na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Anne Kilango Malecela (Mb. Same Mashariki), kwa maelekezo na ushauri wa Kamati ambao umekuwa chachu katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara. Naishukuru pia Kamati kwa kuchambua kwa kina TaarifayaUtekelezaji kwa mwaka wa fedha 2023/24, na kupitisha Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/25. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa ushauri, maelekezo na maoni yaliyotolewa na Kamati yamezingatiwa katika bajeti hii.

  • 6.Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa majukumu yangu umekuwa rahisi kutokana na ushirikiano mkubwa ninaoupata kutoka kwa viongozi wenzangu katika Wizara. Nawashukuru sana Mheshimiwa Mhandisi Godfrey M. Kasekenya, Naibu Waziri; Balozi Mhandisi Aisha S. Amour, Katibu Mkuu, pamoja na Ndugu Ludovick J. Nduhiye, Naibu Katibu Mkuu. Nawashukuru pia Wakuu wa Idara na Taasisi, Mameneja wa Mikoa wa TANROADS, pamoja na Watumishi wa Wizara na Taasisi zake kwa kujituma katika utekelezaji wa majukumu tuliyokasimiwa Wizarani. Tunamuahidi Mheshimiwa Rais na Watanzania wote hatutawaangusha.
  • 7.MheshimiwaSpika,Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya ni Naibu Waziri mnyenyekevu na mchapa kazi. Ninamshukuru Mhe. Rais kwa kuendelea kumuamini, na tunaahidi kudumisha umoja na mshikamano wa Wizara ili kuendelea kutekeleza Ilani ya CCM kwa spidi na viwango. Ninawapongeza wananchi wa Jimbo la Ileje kwa kuchagua Mbunge makini na mchapakazi. Ninawasihi sana wananchi wa Jimbo la Ileje wampe tena nafasi Bungeni mwakani, kwa mitano tena Mheshimiwa Mhandisi Kasekenya ili kazi iendelee.

  • 8.Mheshimiwa Spika, napenda kukupongeza wewe binafsi, kwa kuaminiwa na kuchaguliwa kwa kishindo kuwa Rais wa Muungano wa Mabunge Duniani. Imani hii uliyooneshwa kimataifa inaakisi uwezo mkubwa ulionao katika uongozi wa Bunge letu Tukufu pamoja na masuala ya kimataifa.Umeweza majukumu haya mazito yenye kuleta heshima kubwa kwa nchi yetu. Nawaomba wananchi wa Jimbo la Mbeya Mjini waendelee kuwa watulivu na wakupe mitano tena mwakani, kwani wamepata bahati ya kukupata wewe kiongozi hodari na adimu kwa Mbeya. Hongera sana Mheshimiwa Spika.

Nampongeza pia Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu, Naibu Spika, kwa kuendelea kutekeleza vyema wajibu wake katika kukusaidia kusimamia na kuliongoza Bunge letu. Nawapongeza Mwenyekiti wa Bunge Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, pamoja na Wenyeviti wapya wa Bunge waliochaguliwa hivi karibuni Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama na Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika. Hongereni sana Waheshimiwa Wenyeviti.

  • 9.Mheshimiwa Spika, kwa dhati kabisa napenda kuwashukuru wananchi wa Jimbo langu la Karagwe, kwa ushirikiano wanaoendelea kunipatia katika kuwatumikia, pamoja na kutekeleza jukumu la kuwawakilisha humu Bungeni. Ninawaahidi kuwa nitaendelea kuwatumikia

kwa nguvu na maarifa yangu yote, ili kuhakikisha Wilaya yetu ya Karagwe inapata maendeleo tunayopenda. Asanteni sana Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Karagwe mkiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Cde. Rwamugata, kwa kuwa humu Bungeni leo kuwawakilisha wana Karagwe wenzetu kwenye Bajeti ya Wizara ya Ujenzi.

  • 10.Mheshimiwa Spika, namshukuru pia mke wangu mpendwa Jennifer, (A.K.A Mama Alaska) pamoja na watoto wangu Santo, Solana, Sankara na Samora; kwa namna wanavyonitia moyo, na kuniombea kwa Mwenyezi Mungu, ili niweze kutekeleza majukumu yangu kwa ufanisi.
  • 11.Mheshimiwa Spika, Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Serikali leo tunaye humu Bungeni. Kwa nafasi yangu ya mlezi wa madereva wote wa Serikali nchini, nitumie fursa hii kuwapongeza madereva wa Serikali kwa majukumu yao katika kuendesha na kutunza vyombo vya moto vya Serikali. Nitoe wito kwa madereva hawa kuendelea kuzingatia maadili ya utumishi wa umma. Ninawataka wale wachache wanaoharibu taswira nzuri ya madereva wa Serikali, kwa vitendo vilivyo kinyume na maadili, waache mara moja.

  • 12.Mheshimiwa Spika, napenda pia nichukue fursa hii kuwangeza Vijana wa Jangwani (Young Africans) kwa kuvishwa Taji la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Niwapongeze pia kwa kuchukua ubingwa mara 3 mfululizo na kuweka historia ya kuchukua ubingwa mara 30 tangu kuanzishwa kwa ligi. Imekuwa timu ya pekee hapa nchini kuweka historia hii.

B.MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA 6

  • 13.Mheshimiwa Spika, mwezi Machi 2024, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, alitimiza miaka 3 madarakani. Katika kipindi hicho cha uongozi wake mafanikio makubwa yamepatikana.

Ujenzi wa Barabara

  • 14.Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipoingia madarakani Machi 2021, mtandao wa barabara za lami ulikuwa kilometa 10,830.2. Hadi kufikia Machi 2024, mtandao wa barabara za lami umeongezeka na kufikia kilometa 12,028.7. Katika kipindi cha miaka 3 ya Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani, miradi ya barabara 25 zenye jumla ya kilometa 1,198.5 imekamilika kujengwa katika mikoa mbalimbali nchini. Barabara hizo ni:
  • i.Ujenzi wa barabara ya Tabora (Usesula) Koga Mpanda; (Lot 2): Komanga Kasinde (km 120) mkoani Tabora;
  • ii.Ujenzi wa barabara ya Tabora (Usesula) Koga Mpanda; (Lot 3): Kasinde Mpanda (km 118) mkoani Katavi;

  • iii.Ujenzi wa barabara ya Tabora (Usesula) Koga Mpanda (Lot 1): Usesula Komanga (km 115) mkoani Tabora;
  • iv.Ujenzi wa barabara ya Sumbawanga Matai Kasanga Port (km 107) mkoani Rukwa;
  • v.Ujenzi wa barabara ya Nyahua Chaya (km 85.4) mkoani Tabora;
  • vi.Ujenzi wa barabara ya Mbinga Mbamba Bay (km 66) mkoani Ruvuma.
  • vii.Ujenzi wa barabara ya Kidahwe Kasulu (km 63) mkoani Kigoma;
  • viii.Ujenzi wa barabara ya Nyamuswa Bunda Bulamba (km 55) mkoani Mara;
  • ix.Ujenzi wa barabara ya Njombe Moronga (km 53.9) mkoani Njombe;
  • x.Ujenzi wa barabara ya Moronga Makete (km 53.5) mkoani Njombe;
  • xi.Ujenzi wa barabara ya Mpemba Isongole (km 51.2) mkoani Songwe;
  • xii.Ujenzi wa barabara ya Makutano Natta Mugumu (sehemu ya Makutano Sanzate (km 50) mkoani Mara;
  • xiii.Ujenzi wa barabara ya Lusitu Mawengi (km 50) mkoani Njombe;
  • xiv.Ujenzi wa barabara ya Nyakanazi Kakonko (Kabingo

- km 50) mkoani Kigoma;


  • xv.Ujenzi wa barabara ya Loliondo Mto wa Mbu (sehemu ya Waso Sale Jct) (km 50) mkoani Arusha;
  • xvi.Ujenzi wa barabara ya ChunyaMakongolosi (km 39) mkoani Mbeya;
  • xvii.UjenziwabarabarayaRudewaKilosa(km24) mkoani Morogoro;
  • xviii.Upanuzi wa barabara ya Kimara Kibaha (km 25.7) pamoja na madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji mkoani Dar es Salaam;
  • xix.Ujenzi wa barabara, sehemu ya KusenyiSuguti (km 5) mkoani Mara;
  • xx.Ujenzi wa barabara ya Ardhi Makongo Goba (Sehemu ya Ardhi Makongo -km 5) mkoani Dar es Salaam;
  • xxi.Upanuzi wa barabara ya Morocco Mwenge (km 4.3) mkoani Dar es Salaam;
  • xxii.Ujenzi wa barabara ya Tegeta Kibaoni Wazo Hill Goba Mbezi/Morogoro Road (Mbezi Mwisho); sehemu ya Wazo Hill Madale (km 4.2) mkoani Dar es Salaam;
  • xxiii.Ujenzi wa barabara ya Tungi Kibada (km 3.8) mkoani Dar es Salaam;
  • xxiv.Ujenzi wa barabara ya Banana - Kitunda - Kivule - Msongola, sehemu ya Kitunda Kivule (km 3.2) mkoani Dar es Salaam; na
  • xxv.Upanuzi wa daraja la Gerezani na barabara ya maingilio (km 1.3) mkoani Dar es Salaam.

Katika kipindi hicho cha miaka 3 tangu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameingia madarakani, jumla ya miradi ya barabara 74 zenye urefu wa kilometa 3,794.1 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Kati ya miradi ya barabara hizo 74, utekelezaji wa miradi 12 umefikia asilimia 70 au zaidi, na miradi 62 utekelezaji wake upo chini ya asilimia 70. Miradi hiyo imeoneshwa katika Aya ya 17 ya kitabu cha Hotuba ya Bajeti ya Wizara.

Ujenzi wa Madaraja Makubwa

  • 15.Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka 3 ya Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani, madaraja makubwa 8 yamekamilika kujengwa. Madaraja hayo ni:
  • i.Daraja la Wami mkoani Pwani;
  • ii.Daraja la Tanzanite mkoani Dar es Salaam;
  • iii.Daraja la Gerezani mkoani Dar es Salaam;
  • iv.Daraja la Mpwapwa mkoani Dodoma;
  • v.Daraja la Kiyegeya mkoani Morogoro;
  • vi.Daraja la Ruhuhu mkoani Ruvuma;
  • vii.Daraja la Kitengule mkoani Kagera; na
  • viii.Daraja la Msingi mkoani Singida.

Katika kipindi hicho, ujenzi wa madaraja makubwa 5 upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kama ifuatavyo:


  • i.Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo – Busisi) mkoani Mwanza, 88% na tunalenga likamilike kufikia mwaka huu Disemba 2024;
  • ii.Daraja la Mbangala mkoani Mtwara, 66%;
  • iii.Daraja la Pangani mkoani Tanga, 23%;
  • iv.Daraja la Mbambe mkoani Pwani, 25%; na
  • v.Daraja la Simiyu mkoani Mwanza, 15%.

Miradi ya Viwanja vya Ndege

  • 16.Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya 6 imekamilisha ujenzi wa viwanja vya ndege 3 katika kipindi cha miaka 3 ya Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani, ambavyo ni viwanja vya ndege vya Songea, Mtwara na Songwe. Katika kipindi hicho, Serikali imeendelea na utekelezaji wa miradi ya viwanja vya ndege

7 ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Viwanja hivyo ni: Msalato Airport (56.9% kwakaziza ujenzi wa miundombinu ya kutua na kurukia ndege) na (22.56% kwa kazi za ujenzi wa jengo la abiria na majengo mengine); Musoma Airport (55%); Iringa Airport (90%); Kigoma Airport (Awamu ya III, 3.7%); Sumbawanga Airport (8.4%); Shinyanga Airport (11%); na Tabora Airport (Awamu ya III, 38%).


Taratibu za manunuzi zinaendelea kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Lake Manyara, Iringa (Awamu ya II) na kiwanja cha ndege cha Tanga.

Miradi ya Vivuko (TEMESA)

  • 17.Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya 6 imepata mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za vivuko kupitia TEMESA. Katika kipindi cha kuanzia Machi 2021 hadi Mei 2024 Wizara imeendelea na ujenzi wa vivuko vipya 8 ambavyo vipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Vivuko hivyo vikikamilika vitatoa huduma katika maeneo ya Bwiro – Bukondo (Ukerewe), Kisorya (Bunda) – Rugezi (Ukerewe), Ijinga – Kahangala (Magu), Nyakaliro – Kome (Sengerema), Buyagu (Sengerema) – Mbalika (Misungwi), Mafia – Nyamisati (Rufiji) na Magogoni (Ilala) – Kigamboni (Kigamboni). Serikali itahakikisha mkandarasi M/S Songoro Marine analipwa fedha zote ili akamilishe ujenzi wa vivuko hivi ndani ya mwaka huu. Kwa mwezi Mei pekee, mkandarasi huyo amelipwa jumla ya Shilingi bilioni 1.526.

Miradi ya Nyumba na Majengo ya Serikali (TBA)

  • 18.Mheshimiwa Spika, mafanikio makubwa yamepatikana katika kipindi cha miaka 3 ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ujenzi wa nyumba na majengo kupitia TBA. Sheria iliyoanzisha TBA

imehuishwa ili kuruhusu TBA kushirikiana na sekta binafsi. Uhuishwaji huu umeleta mabadiliko kwenye majukumu ya TBA ikiwemo kuweza kuuza nyumba kwa watu binafsi. Hali hii itaiwezesha TBA kushirikiana na Sekta Binafsi katika kuendeleza milki nchini na kutafuta vyanzo vya fedha kama mikopo kwani miradi yote ambayo itaendelezwa kibiashara itaweza kupangishwa au kuuzwa kwa watu wote kulingana na hali ya soko. Hii itasaidia TBA kujiendesha na kupunguza utegemezi wa ruzuku.

  • 19.Mheshimiwa Spika, kupitia uhuishwaji huu, TBA inatarajia kujenga jumla ya nyumba 1,056 katika maeneo

5 Jijini Dar es Salaam. TBA pia imeandaa orodha ya maeneo yaliyoiva kwa uwekezaji katika mikoa ya Dodoma (12), Arusha (3), Mwanza (2), Shinyanga (1), Singida (1) na Geita (1) na kuyatangaza kwa umma kwa ajili ya miradi ya ubia. Vilevile, TBA imeanza kushirikiana na Taasisi za kifedha katika kutafuta mikopo ya miradi yake mbalimbali ya kibiashara ikiwemo Canadian (Masaki) na Magomeni Kota, ambapo Benki ya CRDB, NMB, TIB na BOA Benki zimeshaonesha nia ya kutoa mkopo wa ujenzi, na mkopo kwa wanunuzi wa nyumba “Mortgage Financing” katika mfumo wa “Pre – Sale”.


Ukusanyaji wa Madeni ya TBA

  • 20.Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/24 TBA iliingia na deni lenye jumla ya Shilingi bilioni

14.35. Kutokana na jitihada kubwa zilizofanywa na Wizara kupitia TBA katika kipindi tajwa, TBA imefanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi bilioni4.3.Hiinisawa na 30% ya malimbikizo ya deni. Hivyo, deni lililobaki ni Shilingi bilioni 10.05. Nitoe wito kwa wapangaji wote kuhakikisha kuwa wanalipa kodi za pango kwa wakati ili kuepusha usumbufukwaonakwaTBA.TBAinaendelea na jitihada za kufuatilia ulipaji wa madeni hayo kwa kutumia dalali wa mahakama ili fedha hizo zitumike kukarabati nyumba zilizopo, na kujenga nyumba mpya ili kukidhi mahitaji yaliyopo.

  • 21.Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika ukusanyaji wa madeni ya TBA, kupitia zoezi hilo kuna baadhi ya wadaiwa walikwazika. Ukusanyaji wa madeni hayo ni maelekezo ya Bunge letu tukufu na CAG, hivyo tunawaomba mtuvumilie wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo kwani ni zoezi endelevu. Ni matarajio yangu kuwa baada ya kukamilika kwa zoezi hili TBA itaweza kuboresha huduma zake ili wapangaji wake wafurahie maisha bora ndani ya nyumba za TBA, na kujenga majengo mengi zaidi kulingana na mahitaji.

Udhibiti Uzito wa Magari

  • 22.Mheshimiwa Spika, kuzuia uharibifu wa miundombinu ya barabara ni jambo la lazima na zoezi endelevu kwa kuwa tabaka la lami la barabara hujengwa kwa gharama kubwa.
  • i.Wizara ina mpango wa kufunga mizani yenye teknolojia inayopima uzito wa magari yakiwa kwenye mwendo (Weigh in Motion System), katika vituo vyote vya mizani nchini ili kutatua changamoto ya msongamano wa magari katika vituo vya mizani. Katika mwaka 2024/25 mizani 32 itajengwa. Lengo ni kuwa na jumla ya mizani 110 ifikapo mwaka 2026/27. Mizani hii yenye teknolojia ya kisasa hufungwa barabarani ili kuchuja magari ambayo hayajazidi uzito na kuyaruhusu kuendelea na safari, hivyo msafirishaji hatalazimika kuingia katika kituo cha mzani endapo gari lake halitabainika kuzidi uzito katika mizani ya WIM.

Mizani ya aina hii itasaidia kwa sehemu kubwa kupunguza msongamano wa magari barabarani na katika vituo vya mizani, na kupunguza muda wa safari kwa magari yaliyobeba mizigo inayokwenda nje ya nchi (Transit Vehicles) na ndani ya nchi, na hivyo kuendelea kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.


  • ii.Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS ilianzisha na kutekeleza utaratibu wa magari ya mafuta (fuel tankers) na makasha yenye rakili (sealed containers) kupima uzito katika vituo 3 tu vya mizani katika kila ushoroba. Utaratibuhuu umesaidiakupunguza muda wa safari pamoja na msongamano wa magari katika vituo vya mizani.
  • iii.Wizara imefanya marekebisho katika maeneo hatarishi yaliyopo barabara kuu ya kwenda Zambia, ili kupunguza ajali za barabarani; eneo la Mlima Kitonga lenye urefu wa km 7.6 kwa kufanya upanuzi wa kona 5 zenye urefu wa km 1.6 na upana wa mita 5. Ujenzi utaendelea kwa awamu hadi Mlima wote wa Kitonga upitike bila shida yoyote. Ujenzi wa maeneo ya maegesho, barabara za dharura na barabara ya mchepuo, yenye urefu wa km 2.8 kwa kiwango cha lami umefanyika ili kutenganisha malori na magari mengine katika eneo la Inyala mkoani Mbeya.
  • 23.Mheshimiwa Spika, hayo ni machache kati ya mengi mazuri ambayo Serikali ya Awamu ya 6, chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeyafanya katika Sekta ya Ujenzi. Hakika, Mheshimiwa Rais Samia

/ni mama na Rais mwenye maono, muonesha njia na mchapakazi. Tunamuombea afya njema na maisha marefu ili aendelee kuiongoza Tanzania yetu kufikia mafanikio

makubwa kijamii na kiuchumi.


C.UHARIBIFU MKUBWA WA MIUNDOMBINU YA BARABARA NA MADARAJA KUTOKANA NA MVUA ZA EL-NINO NA KIMBUNGA HIDAYA

  • 24.Mheshimiwa Spika, nchi yetu imeathirika na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yameleta athari za kimazingira katika maeneo mbalimbali dunia nzima. Athari hizo kwa Tanzania zimejidhihirisha kupitia mvua kubwa za El – Nino zilizonyesha kwa takriban miezi 9 mfululizo kuanzia Septemba 2023 hadi hivi sasa mwezi Mei. Mvua hizo zimesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara na madaraja kote nchini. Mikoa iliyoathiriwa zaidi ni Lindi, Ruvuma, Morogoro, Singida, Tabora, Dodoma, Kilimanjaro, Songwe, Simiyu, Mbeya, Rukwa, Mwanza, Dar es Salaam, Pwani, Arusha, Njombe, Iringa, Mtwara, Shinyanga na Manyara.
  • 25.Mheshimiwa Spika, vilevile, kimbunga Hidaya kiliyakumba maeneo ya pwani ya nchi yetu na kusababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Pwani. Mvua kubwa zilizoambatana na kimbunga hiki, zilisababishakukatika kwa mawasiliano bainayamikoayaPwani naLindi eneo la Mikereng‘ende, Songas, Somanga na Matandu – Nangurukuru. Maeneo mengine yaliyoathirika kwa kiasi kikubwa ni katika barabara ya Nangurukuru – Liwale

(daraja la Miguruwe, eneo la Zinga na eneo la Mlowoka); Kiranjeranje – Namichiga (daraja la mto Mbwemkuru na daraja la Kigombo) pamoja na Tingi – Kipatimu(eneola mto Liomanga na eneo la mto Chumo).

Kwa ujumla, uharibifu uliotokea katika barabara ya Mtwara – Lindi – Dar es Salaam ni mkubwa, na hivyo barabara yote inatakiwa kujengwa upya. Tayari manunuzi kwa ajili ya ukarabati kwa kiwango cha lami wa kipande cha barabara ya Mtwara - Mingoyo yapo katika hatua za mwisho, na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Julai 2024.

  • 26.Mheshimiwa Spika, Serikali ilichukua hatua za haraka kuhakikisha kuwa mawasiliano katika maeneo yaliyoathirika yanarejea. Hadi Mei 2024 kiasi cha Shilingi bilioni 72 zilitolewa kwa ajili ya kurejesha mawasiliano. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za dharura. Tathmini ya jumla iliyofanyika imeonesha kuwa mahitaji halisi kwa ajili ya miundombinu iliyoathirika na mvua za El – Nino na Kimbunga Hidaya ni Shilingi trilioni 1.07. Serikali inasubiri taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuhusu kumalizika kwa msimu wa mvua, kwa ajili ya kuendelea na ukarabati na matengenezo ya maeneo yaliyoathiriwa.

D.MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGONABAJETI YA WIZARA NA TAASISI ZAKE KWA MWAKA WA FEDHA 2023/24

Ushiriki wa Wazawa (Local Content) katika Utekelezaji wa Miradi Mikubwa ya Ujenzi

  • 27.Mheshimiwa Spika, Sekta ya Ujenzi ni mojawapo ya Sekta muhimu zinazochangia kwa kiasi kikubwa katika Pato la Taifa. Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, wastani wa mchango wa Sekta katika Pato la Taifa katika kipindi cha miaka kumi (2012 – 2022) ni 14%. Sekta hii imekuwa ikikua kwa wastani wa 12% kwa mwaka kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita. Serikali imekuwa ikitenga fedha nyingi kila mwaka kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Miradi hiyo hutekelezwa na makandarasi kutoka ndani na nje ya nchi. Hata hivyo, pamoja na kutengewa kiasi kikubwa cha fedha, uchambuzi wa taarifa za usajili wa miradi ya ujenzi kwa miaka 10, (2013 – 2023), umebaini ushiriki mdogo wa makandarasi wazawa katika miradi hiyo.
  • 28.Mheshimiwa Spika, kwa mujibu watakwimuza Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), kati ya jumla ya miradi 36,839, Wazawa walitekeleza miradi 35,351 sawa na asilimia 95.9 ya miradi hiyo katika kipindi cha 2013 - 2023. Hata hivyo, miradi iliyotekelezwa na wazawa ni

midogo midogo yenye thamani ya Shilingi trilioni 23.749,


sawa na 38.5% ya thamani ya miradi yote iliyosajiliwa na kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10, ambayo ni Shilingi trilioni 61.638. Hivyo, makandarasi wa nje ambao ni takriban asilimia 4.1 walitekeleza miradi michache lakini yenye thamani kubwa ( yaani 61.5% ya thamani ya miradi yote).

Hii inaonesha kuwa asilimia kubwa ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inawanufaisha wageni kutoka nje ya nchi kuliko Wazawa. Sababu kubwa inayochangia hali hii ni uwezo mdogo wa makandarasi wa ndani wa kifedha, mitambo na wataalam; hivyo inakuwa vigumu kwao kushindana kwenye zabuni za kazi na makandarasi kutoka nje.

  • 29.Mheshimiwa Spika, kutokana nachangamotohizi za makandarasi wa ndani, Wizara imedhamiria kuwawezesha makandarasi wazawa kushiriki kwenye kazi kubwa za ujenzi kuanzia usanifu, manunuzi, ujenzi, matengenezo na ukarabati. Uwezeshaji wa wazawa utaleta manufaa ikiwemo kukuza biashara za wazawa; kupunguza matumizi ya fedha za kigeni; kuongeza ajira na ujuzi kwa wataalam wa ndani, pamoja na kujenga uwezo wa kampuni za ndani kuweza kushindana kimataifa.

  • 30.Mheshimiwa Spika, tarehe 21 Novemba, 2023 niliitisha mkutano wa mashauriano na makandarasi pamoja na washauri elekezi wa ndani kutoka mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar. Lengo la mkutano huo lilikuwa kupata maoni na ushauri kutoka kwa makandarasi wenyewe, kuhusu changamoto walizonazo na utayari wa Serikali kuzitafutia suluhu. Baada ya mkutano huo, niliunda timu ya wataalam ili wachambue changamoto hizo na kuandaa Mkakati wa Kuongeza Ushiriki wa Wazawa katika Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (Local Content Strategy). Timu hiyo tayari imekamilisha kazi na imeandaa mapendekezo ya kufanyiwa kazi ya muda mfupi, wa kati na muda mrefu. Mapendekezo hayo ni pamoja na:
  • i.Kurekebisha vipengele kwenye makabrasha ya zabuni za TANROADS ambavyo vina masharti magumu bila sababu za msingi, na kusababisha wazawa washindwe kuvitimiza wakati wa kuomba zabuni, na hivyo kuondolewa kwenye mchakato wa zabuni;
  • ii.Serikali kuanzisha mpango maalum wa kuwajengea

uwezo na kuwaendeleza makandarasi na wataalam wa ndani. Lengo ni kuwawezesha wakue na wawe na


uwezo wa kushindana na makandarasi wa nje, hata kuwa na uwezo wa kuomba kazi nje ya nchi na hivyo kupanua wigo wa ajira kwa watanzania; na

  • iii.Sheria ya Manunuzi ya Umma kuboreshwa ili iongeze kiasi cha fedha kwa miradi ya kutekelezwa na wazawa peke yao kutoka kiasi cha Shilingi bilioni 10 cha sasa hadi Shilingi bilioni 50.
  • 31.Mheshimiwa Spika, hadi Mei 2024 tayari Serikali imetekeleza mapendekezo hayo kwa kufanya yafuatayo:
  • i.TANROADS kwa kushirikiana na PPRA wanaendelea na taratibu za kuboresha/kurekebisha vipengele kwenye makabrasha ya zabuni vilivyokuwa vikwazo kwa makandarasi wazawa;

Vipengele vilivyoboreshwa ni pamoja na:

Kupunguza kiwango cha mapato ghafi (Average Annual Turnover);

  • a)KutumiwakwaTender/ Bid Securing Declaration

badala ya Tender/ Bid security;

  • b)Kutumia Performance Bonds/ Performance Securing Declaration badala ya Performance Bank Guarantee;

  • c)Kutambua uzoefu wa wataalam badala ya uzoefu wa kampuni kwa ajili ya kazi zinazofanana (specific experience in similar projects).
  • ii.Wizara imetenga miradi maalum ya kuwajengea uwezo makandarasi wa ndani na makandarasi wanawake; na
  • iii.Wizara ya Fedha imerekebisha Sheria ya Manunuzi ya Umma kwa kuongeza wigo wa thamani ya miradi ya kutekelezwa na wazawa peke yao. Imependekeza kiwango kipande kutoka Shilingi bilioni10zasasa hadi Shilingi bilioni 50.

Nitumie fursa hii kumshukuru sanaMheshimiwaWaziri Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, na Wizara ya Fedha anayoiongoza kwa ushirikiano wa karibu kwenye utekelezaji wa mikakati ya kuwezesha wazawa ambayo utekelezaji wake tumeanza mara moja.

  • 32.Mheshimiwa Spika, sambamba na kuwajengea uwezo Makandarasi Wazawa, Wizara ina mkakati wa kuwajengea uwezo Makandarasi wanawake kwa kuongeza ushiriki wao katika miradi mikubwa ya ujenzi wa barabara. Hadi sasa Wizara imetenga jumla ya kilometa 20 za ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kwa ajili ya Makandarasiwanawakepekee.Kazihizizitagawanywa

katikasehemuzakilometatanotanoambapo


Makandarasi wanawake pekee yao ndio wataomba kazi hizo. Hivi sasa miradi hii ipo kwenye hatua ya ununuzi.

  • 33.Mheshimiwa Spika, nitoe wito kwa makandarasi wazawa kufanya kazi kwa weledi na utaalam, ili mikakati iliyowekwa na Serikali isitafsiriwe kama mteremko. Hii ni kwa kuwa baadhi ya makandarasi wazawa waliopewa miradi ya upendeleo wameikatisha tamaa Serikali kwa kutokuwa waadilifu, usimamizi usioridhisha wa miradi na kutumia muda mrefu katika utekelezaji wa miradi. Rai yangu kwa makandarasi wa ndani ni kushiriki kikamilifu, kwa uzalendo na uadilifu mkubwa katika ujenzi wa taifa letu. Vilevile mjiepushe na vitendo vya rushwa, tekelezeni mradi kwa ubora uliotegemewa, ili kutoangusha dhamira hii njema ya Mheshimiwa Rais Dkt.SamiaSuluhu Hassan ya kuwainua kiuchumi. Kazi kwenu makandarasi wazawa.
  • 34.Mheshimiwa Spika, napenda nimpongeze kwa dhati Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Taifa Mary Chatanda kwa ufuatiliaji wa karibu kuhusu fursa hizi kwa makandarasi wanawake.

Kujenga Uwezo wa Ndani ya Taasisi na Wastaafu Wabobezi Katika Usimamizi wa Miradi

  • 35.Mheshimiwa Spika, TANROADS inatumia Kitengo chake cha ndani cha Ushauri wa Kihandisi (TECU) katika usanifu na usimamizi wa miradi ya ujenzi wa barabara na madaraja. Lengo ni kujenga uwezo wa taasisi zetu kusimamia miradi badala ya kutegemea wataalam nje. Hii imesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za usimamizi wa miradi pamoja na muda unaotumiwa katika ununuzi wa wahandisi washauri. TECU imeshiriki kwa mafanikio makubwa katika utekelezaji wa miradi kadhaa ya kimkakati, ikiwemo Mradi wa Uzalishaji wa Umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Njia 8 ya Kimara – Kibaha (km19.2), Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Geita, na ujenzi wa kiwanda cha sukari cha Mbigiri.

Vilevile, Wizara kupitia taasisi zake ERB na TANROADS inaandaa utaratibu wa kutumia wataalam wa ndani waliostaafu (retired but not tired) katika ujenzi na matengenezo ya barabara. TECU inaendelea kuwatumia wahandisi wabobezi waliostaafu katika usanifu na usimamizi wa miradi. Hii imesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza utegemezi wa wahandisi washauri kutoka nje. Jambo hili la kutumia wastaafu pia linatoa fursa kwa


wataalam wanaochipukia na ngazi ya kati kujifunza kutoka kwa wastaafu wabobezi ambao wako nyumbani wakati ujuzi wao bado unahitajika katika ujenzi wa taifa letu.

Upatikanaji wa Malighafi za Ujenzi

  • 36.Mheshimiwa Spika, kuhusu upatikanaji wa malighafi za ujenzi, ikiwemo changarawe, mchanga, na kokoto, Wizara ya Ujenzi inaendelea na mazungumzo na Wizara ya Madini. Mazungumzo hayo yanalenga kupata namna bora ya kutatua changamoto kubwa ya upatikanaji wa malighafi hizo. Changamoto kubwa ni uwepo wa vishoka wanaoshikilia maeneo yenye malighafi za ujenzi na kutoza fedha nyingi. Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali wale wote watakaobainika kujihusisha na mchezo huo mchafu. Dhamira ya Wizara ni kuwa kwa kadri inavyowezekana maeneo hayo yamilikishwe TANROADS ili kuwezesha miradi mingi ya barabara kutekelezwa kwa wakati, na kupunguza gharama za ujenzi.

Nitumie fursa hii kumshukuru kwa dhati Mhe. Antony Mavunde, Waziri wa Madini kwa ushirikiano anaotupatia katika kuhakikisha kuwa malighafi za ujenzi zinapatikana kwa gharama nafuu na hivyo kupunguza gharama za miradi.Hii itawezekana iwapo TANROADS itakuwa na

maeneo ya kuchimba madini ya ujenzi na kuondokana na


hali ya sasa ya vishoka wanaopandisha gharama za ujenzi.

Utekelezaji wa Miradi kwa Utaratibu wa Kushirikisha Sekta Binafsi (PPP)

  • 37.Mheshimiwa Spika, ujenzi wa miradi ya miundombinu hasa ya barabara na madaraja inaigharimu Serikali kiasi kikubwa cha fedha. Ili kuipunguzia Serikali gharama kubwa za utekelezaji wa miradi hiyo, Wizara imeanza kuishirikisha sekta binafsi kwa utaratibu wa PPP. Lengo la kutumia utaratibu huu ni kujenga miundombinu na inasaidia kutekeleza miradi kwa wakati. Katika miradi ya barabara, Serikali inatekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya Kibaha – Chalinze – Morogoro – Dodoma (Expressway) yenye urefu wa kilometa 423.8 kwa mfumo wa kulipia (Toll Road System). Mradi huu umegawanywa katika sehemu 3 kama ifuatavyo:
  • i.Sehemu ya Kibaha – Chalinze (km 78.9), kazi inayoendelea ni uchambuzi waProposals(Evaluation of Technical & Financial Proposals) wa wawekezaji waliofaulu vigezo vya kupatiwaRequest for Proposals ya kutekeleza mradi huu.
  • ii.Kwa sehemu ya Chalinze – Morogoro yenye urefu wa

kilometa 84.9, Mshauri Elekezi yupo katika hatua za mwisho kukamilisha kazi ya Upembuzi Yakinifu.


  • iii.Kwa sehemu ya Morogoro – Dodoma (km 260) usanifu wa kina wa kawaida (Conventional Design) uko katika hatua za mwisho kukamilika. Usanifu utatumika kujenga Concept ya mradi wa PPP.

Utekelezaji wa Miradi kwa Utaratibu wa EPC+F

  • 38.MheshimiwaSpika, Serikali imepanga kutekeleza miradi 7 ya ujenzi wa barabara zenye jumla ya urefu wa kilometa 2,035 zenye kugharimu Shilingi trilioni 3.7 kwa utaratibu wa Engineering, Procurement, Construction and Finance (EPC+F).EPC+Fnimfumo wautekelezaji wa miradikwakutumiamakandarasiambao wanahusika katika taratibu za kumpata mgharamiaji wa mradi kwa njia ya mikopo. Mfumo huu kwa nchi yetu ni mpya na lengo la kutumia mfumo huu ni kupunguza utegemezi wa fedha za ndani katika ujenzi wa barabara. Miradi hiyo 7 imeoneshwa katika Aya ya 40 ya kitabu cha Hotuba. Serikaliinaendeleanamazungumzonamakandarasi kuhusu ugharamiaji wa miradi yote 7 ili kupata fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hii. Napenda kuwahakikishia WaheshimiwaWabungekuwadhamira yaSerikali ya kutekeleza miradi hii ya EPC+F bado ipo palepale.
  • 39.MheshimiwaSpika,naombasasanielezekwa

muhtasari utekelezaji wa bajeti iliyoidhinishwa na Bunge lako Tukufu kwa mwaka wa fedha 2023/24.


Bajeti ya Matumizi ya Kawaida

  • 40.Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/24, Wizara ya Ujenzi ilitengewa jumla ya Shilingi 48,395,392,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 43,958,274,000.00 zilikuwa ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake na Shilingi 4,437,118,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi zake.

Hadi Aprili 2024 jumla ya Shilingi 48,665,781,258.75 zilikuwa zimetolewa na HAZINA kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida.

Bajeti ya Miradi ya Maendeleo

  • 41.Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/24,WizarailitengewaShilingi 1,419,843,057,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 2,699,800,000.00 zilihamishiwa Wizara ya Uchukuzi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Viwanja vya Ndege. Hivyo, WizarayaUjenziilibakiwana Shilingi 1,417,143,257,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

HadiAprili2024fedhazilizopokelewaniShilingi


1,421,842,330,490.81 ya fedha zilizotengwa kwa mwaka wa fedha 2023/24.

Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2023/24

  • a.Miradi ya Barabara na Madaraja Iliyotekelezwa
  • 42.Mheshimiwa Spika, maelezo kuhusu utekelezaji wa miradi ya barabara na madaraja yameoneshwa katika Aya ya 42 - 129 ya kitabu cha Hotuba yangu.

b.Miradi ya Barabara na Madaraja Iliyosainiwa Mwaka wa Fedha 2023/24

  • 43.Mheshimiwa Spika, pamoja na utekelezaji wa miradi inayoendelea, Serikali imeamua kutekeleza miradi mipya ya ujenzi wa barabara ili kuhakikisha wananchi wanatumia miundombinu bora ya barabara. Katika mwaka wa fedha 2023/24, mikataba ya ujenzi/ukarabati/usanifu wa miradi 25 mipya ya barabara, madaraja na mizani ilisainiwa. Miradi hiyo ni:
  • i.Maboresho ya miundombinu ya mabasi yaendayo haraka iliyojengwa katika Awamu ya Kwanza (Kimara
  • Kivukoni; Kawawa Gerezani na Kawawa- Morocco zenye jumla ya km 20.9). Maboresho yanahusisha ukarabati wa sehemu ya Obama Drive pamoja na

barabara iendayo Stendi ya mabasi ya Kivukoni na barabara ya Msimbazi;

  • ii.Ujenzi wa daraja la Simiyu (Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza) (m 150) na barabara unganishi kilometa 3.0 kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa usanifu na ujenzi;
  • iii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Tarime - Mugumu (km 86); Sehemu ya Tarime Mogabiri (km 9.3), Nyamongo Mugumu (km 48.15) pamoja na barabara ya kuelekea Mugumu Roundabout (km 3.6);
  • iv.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Bigwa Matombo Mvuha (km 78) pamoja na ujenziwa daraja la Ruvu (m 64) na daraja la Mvuha (m 60);
  • v.Ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Nachingwea
  • Ruangwa Nanganga (km 106); sehemu ya Nachingwea Ruangwa (km 57.6);
  • vi.Ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Likuyufusi Mkenda (km 122.5); sehemu ya Likuyufusi Mhukuru (km 60);
  • vii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kibada
  • Mwasonga Tundwisongani Jct/Tundwisongani Kimbiji (km 41); sehemu ya Kibada Mwasonga (km 26.7) na Songani Jct Kijata Jct;
  • viii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Ubena Zomozi - Ngerengere (km 11.6);

  • ix.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kitai Lituhi (km 84.5); sehemu ya Ruanda Ndumbi Port (km 50) kwa kiwango cha lami;
  • x.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Ifakara
  • Kihansi (km 124); Sehemu ya Mbingu Chita JKT (km 37.5);
  • xi.Ujenzi wa Mizani ya Kizengi pamoja na uwekaji taa za barabarani katika barabara ya Tabora - Nyahua Chaya;
  • xii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Iringa (Ipogolo) - Kilolo (km 33.61);
  • xiii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemuya Kongwa Jct Ngambi Mpwapwa (km 32) na Mpwapwa - Gulwe

- Kibakwe (km 46.9);

  • xiv.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kagwira
  • Ikola Karema Port (km 112); Sehemu ya Kagwira Kasekese (km 54.15);
  • xv.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kagwira
  • Ikola Karema Port (km 112); Sehemu ya Kasekese - Ikola (km 56.91);
  • xvi.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Same - Kisiwani - Mkomazi (km 100.5); sehemu ya Lot 2: Ndungu Mkomazi (km 36);
  • xvii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Isongole II Kasumulu Ipyana Katumbasongwe (km 114.3) ikijumuisha barabara ya Ndembo Isoko Spur Road

(km 5.92) na sehemu ya Muungano Ipyana (km 0.66); Lot 1: Isongole II Ndembo (km 46) na Ndembo Spur Road (km 6);

  • xviii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Katumba
  • Mbambo - Tukuyu (km 79.4); sehemu ya Lot 3: KatumbaLupaso (km 35.3);
  • xix.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Katumba Mbambo Tukuyu (km 79.4); sehemuya Lot 4: Mbaka Kibanja (km 20.7);
  • xx.Usanifu na ujenzi kwa kiwango cha lami (Design and Build) wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka (km 50);
  • xxi.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Ntyuka Jct - Mvumi - Kikombo Jct (km 76) na Chololo - Mapinduzi (TPDF HQ) (km 5); sehemu ya Ntyuka Mvumi Hospital - Kikombo (km 53);
  • xxii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kahama
  • Bulyanhulu Jct Kakola (km 73);
  • xxiii.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Matai Kasesya (km 50.6); sehemu ya Tatanda Kasesya (km 25);
  • xxiv.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Dareda
  • Dongobesh (km 60); sehemu ya Dareda Mjini Dareda Mission (km 8);na
  • xxv.Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Sungusila Nzera Nkome Port (km 20.36).

  • 44.Mheshimiwa Spika, maelezo ya utekelezaji wa miradi matengenezo ya barabara na madaraja, vivuko, nyumba na majengo ya TBA, pamoja na udhibiti wa uzito wa magari yameoneshwa katika Kitabu cha Hotuba yangu kuanzia Aya ya 133 150.

c.Miradi ya Ujenzi wa Miundombinu ya Viwanja vya Ndege

  • 45.Mheshimiwa Spika, majukumu ya ujenzi wa viwanja vya ndege nchini yamerejeshwa Wizara ya Uchukuzi. Hata hivyo, Wizara kupitia TANROADS inaendelea kutekeleza miradi ya uendelezaji wa viwanja vya ndege ambayo utekelezaji wake umefikia asilimia 40 na zaidi na miradi ambayo ina ufadhili wa Washirika wa Maendeleo. Miradi hiyo ni viwanja vya ndege vya Msalato, Geita, Kigoma, Tabora, Songwe,Mtwara,Sumbawanga,Shinyanga, Iringa, Musoma, Songea, TanganaLakeManyara.Miradi hii ikikamilika viwanja vitarejeshwa TAA kwa ajili ya usimamizi na uendeshaji.

Maelezo ya kina kuhusu utekelezaji wa miradi ya Viwanja vya Ndege yameoneshwa kwa kina katika Kitabu cha Hotuba yangu kuanzia Aya ya 151 159.


E.CHANGAMOTO ZILIZOIKABILIWIZARANA MIKAKATI YA KUZITATUA

  • 46.Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara, zipo changamoto kadhaa ambazo zimechangia kutokufikiwa malengo kwa ufanisi uliokusudiwa. Changamoto hizo na mikakati ya kuzitatua zimeoneshwa katika Kitabu cha Hotuba yangu Aya ya 230.

F.MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

  • 47.Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi imeandaa Makadirio ya Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 kwa kuzingatia vipaumbele vifuatavyo:
  • a)Kufanya matengenezo ya miundombinu ya barabara na madaraja iliyoharibiwa na mvua za El Nino na Kimbunga Hidaya. Serikali inaendelea na majadiliano na wadau wa maendeleo wakiwemo WB na AfDB ili kupata fedha za matengenezo kupitia dirisha la dharura la Contingency Emergency Response Component (CERC). Kipaumbele kitakuwa ni kurejesha miundombinu ya madaraja na makalavati katika maeneo yaliyoathiriwa nchi nzima.
  • b)Kuendelea na utekelezaji wa miradi inayoendelea ambayo ni pamoja na:
  • i.Ujenzi wa barabara za kimkakati zenye kufungua fursa za kiuchumi kama utalii, kilimo, madini, bandari, viwanda, Bwawa la Kufua Umeme la Nyerere;

  • ii.Miradi ya kupunguza msongamano katika miji mikubwa kama vile Jiji la Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya na Dodoma;
  • iii.Ujenzi wa barabara zinazounganisha makao makuu ya mikoa, zinazounganisha na nchi jirani kwa kiwango cha lami pamoja na barabara za ulinzi;
  • iv.Usanifu wa barabara mpya hasa mijini kwa kuzingatia mahitaji ya watumiaji wote wa barabara ikiwemo wanamichezo, watembea kwa miguu na wanaoendesha vyombo visivyo vya moto hususan baiskeli;
  • v.Miradi ya kimkakati ikiwemo kukamilisha ujenzi wa viwanja vya ndege vya Msalato, Geita, Kigoma, Tabora, Songwe, Mtwara, Sumbawanga, Shinyanga, Iringa, Musoma, Songea, Tanga na Lake Manyara;
  • vi.Miradi ya udhibiti wa uzito wa magari ikiwemo kujenga mizani ya Weigh in Motion (WIM) ili kupunguza msongamano wa malori barabarani na kwenye mizani;
  • vii.Miradi ya ujenzi na ukarabati wa vivuko kupitia TEMESA; na
  • viii.Miradi ya nyumba na majengo ya Serikali kupitia TBA.

  • c)Kuendelea na matengenezo ya barabara Kuu na za Mikoa pamoja na madaraja kwa kuwatumia makandarasi wa ndani kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara pamoja na kuhakikisha kuwa barabara zinapitika katika majira yote ya mwaka;
  • d)Kuendelea kuwajengea uwezo wataalam wa ndani kupitia programu mbalimbali kwa lengo la kuongeza wataalam wabobezi wa ndani ili waweze kusimamia miradi mikubwa inayoendelea kutekelezwa nchini (Local content). Hii ni pamoja na kukijengea uwezo Kitengo cha Ushauri Elekezi wa Miradi cha TANROADS (TECU) ili kiendelee kusimamia miradi mikubwa ya kimkakati;
  • e)Kufanya mapitio ya Sera ya Ujenzi (2003) na Sera ya Taifa ya Usalama Barabarani (2009) pamoja na kanuni na miongozo mbalimbali inayohusiana na Sekta ya Ujenzi ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia na tabianchi;
  • f)Kuendelea kuimarisha mifumo ya TEHAMA katika utendaji kazi;
  • g)Kutumia teknolojia za gharama nafuu katika ujenzi wa barabara hususan katika maeneo korofi;
  • h)Kutekeleza Mkakati wa Uimarishaji wa Utendaji kazi wa TEMESA (TEMESA Transformation Strategy 2024 – 2034).

Makadirio ya Bajeti ya Matumizi ya Kawaida

  • 48.Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/25, Wizara ya Ujenzi imetengewa Shilingi 81,407,438,000.00 ikiwa ni Bajeti ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 76,588,233,000.00 ni Bajeti ya Mishahara na Shilingi 4,819,205,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.

Makadirio ya Bajeti ya Miradi ya Maendeleo

  • 49.Mheshimiwa Spika, Bajeti ya Maendeleo kwa Wizara ya Ujenzi ni Shilingi 1,687,888,714,000.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,141,803,989,000.00ni fedha za ndani na Shilingi 546,084,725,000.00 ni fedha za nje. Kati ya fedha za ndani, Shilingi 599,756,467,800.00 ni fedha zilizotengwa kwa ajili ya bajeti ya Mfuko wa Barabara na fedha kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali ni Shilingi 542,047,521,200.00.

Mgawanyo wa fedha za maendeleo pamoja na miradi iliyotengewa fedha ni kama inavyooneshwa katika Kiambatisho Na.1.

  • 50.Mheshimiwa Spika, pamoja na miradi hiyo, Wizara

kupitia TANROADS itaanza utekelezaji wa mradi wa kimkakati wa Ujenzi wa Daraja la Jangwani ambao ni


sehemu ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa maendelezo ya Bonde la Mto Msimbazi. Daraja litakalojengwa lina urefu wa mita 390 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa mita 710 na kina cha mita 15.5 kutoka usawa wa bahari. Daraja hili litakapokamilika litatatua changamoto ya kujaa kwa maji katika barabara ya Dar es Salaam - Morogoro eneo la Jangwani wakati wa mvua na kusababisha kufungwa kwa barabara hiyo mara kwa mara. Tathmini ya zabuni ili kumpata Mkandarasi na Mhandisi Mshauri zinaendelea.

  • 51.Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi ambayo inalenga kuondoa kero ya msongamano wa magari katika majiji. Miradi hiyo ni pamoja na
  • i.Upanuzi wa barabara ya Mwanza - Usagara – Daraja la JPM kuwa njia 4 (km 37): Sehemu ya Mwanza – Usagara (km 22);
  • ii.BRT Awamu ya 3: Mradi huu unahusisha barabara ya Nyerere kuanzia makutano yabarabarayaKivukoni na Mtaa wa Azikiwe hadi Gongolamboto (km 23.33);
  • iii.BRT Awamu ya 4 (km 30.12): Mradi huu unahusisha barabara ya Ali Hassan Mwinyi – Morocco – Mwenge – Tegeta; na kipande cha Mwenge – Ubungo;
  • iv.BRT Awamu ya 5 (km 27.6): Mradi huu unahusisha

barabara ya Mandela kuanzia makutano ya Ubungo –


Bandari, makutano ya Mandela/Tabata – Tabata Segerea na Tabata – Kigogo;

  • v.Upanuzi wa barabara ya Mbagala Rangitatu - Kongowe (km 3.8) na daraja la Mzinga ili kupunguza ajali na kero kubwa ya foleni;
  • vi.Upanuzi wa barabara ya Mwai – Kibaki (Morocco – Shoppers Plaza – Kwa Nyerere – Kawe Roundabout – Africana: km 11.6);
  • vii.Upanuzi wa barabara ya Uyole – Ifisi - Songwe Airport Jijini Mbeya yenye urefu wa kilometa 36 kutoka njia 2 kuwa njia 4;
  • viii.Ukamilishaji wa ujenzi wa barabara ya mzunguko katika Jiji la Dodoma unaohusisha ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya mzunguko wa nje yenye jumla ya urefu wa kilometa 112.92 (Ihumwa Dry Port

– Matumbulu – Nala: km 60.62); na (Nala – Veyula – Mtumba – Ihumwa Dry Port: km 52.3);

  • ix.Ujenzi wa barabara hapa Dodoma ya mzunguko wa ndani (Bahi Round about – Image Round about – Ntyuka Round about na Makulu Round about: km 6.3);
  • x.Ujenzi wa barabara ya mzunguko wa kati hapa Dodoma (Nanenane – Miyuji – Mnadani Sekondari – Mkonze – Ntyuka – Nanenane : km 47.2);
  • xi.Upanuzi wa barabara ya Dodoma – Morogoro eneo la Bunge hadi Mji wa Serikali Mtumba; na

  • xii.Ujenzi wa barabara za mchepuo za Singida (Kisaki – Kititimo – Mtipa – Manga: km 46), Iringa (Stendi ya Igumbilo – Kihesa Kilolo: km 7), Kilimanjaro (Kwa Sadala) na Songea (Namanditi – Changarawe: km14.4).
  • xiii.Ujenzi wa barabara za kupunguza msongamano mkoa wa Morogoro: Msamvu - Kinguluwila km 7; Msamvu- Kihonda km 5; na Msamvu – Mafiga km 3

Ushirikishwaji wa Sekta Binafsi

  • 52.Mheshimiwa Spika, miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara, madaraja, viwanja vya ndege, vivuko na majengo inagharimu fedha nyingi na hivyo kuhitaji uwekezaji mkubwa. Ni dhahiri kuwa, Serikali pekee haitakuwa na uwezo wa kutekeleza miradi hii yote kwa wakati kutokana na ufinyu wa bajeti. Ili kuipunguzia Serikali gharama kubwa za utekelezaji wa miradi hiyo sambamba na kupunguza muda mrefu unaotumika katika kutekeleza miradi, Wizara inakaribisha ushiriki wa sekta binafsi kwa utaratibu wa PPP. Serikali imefanya maboresho makubwa katika Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Sura 103) kwa lengo la kuvutia uwekezaji katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu. Maboresho haya yatasaidia kuhakikisha kuwa mazingira ya uwekezaji yanakuwa rafiki zaidi kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa.

  • 53.Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya Kibaha – Chalinze – Morogoro – Dodoma Expressway kwa utaratibu wa PPP. Serikali inaandaa andiko la ujenzi wa barabara ya TANZAM (kwa toll road system ya utaratibu wa PPP), kuanzia Morogoro – Iringa – Mbeya hadi Tunduma kwa kuanzia na sehemu ya Igawa – Mbeya hadi Tunduma, ambayo kwa kiasi kikubwa itasaidia kupunguza msongamano wa magari katika mpaka wetu na Zambia pale Tunduma, na pia msongamano wa magari katika Jiji la Mbeya.
  • 54.MheshimiwaSpika,miradimingineiliyoainishwa na Wizara ambayo inawezekana kutekelezwa kwa utaratibu wa PPP ni:
  • i.Barabara za Mzunguko Dar es Salaam:
  • Outer Ring Road(Bunju – Kibamba – Pugu Kajiungeni – Mzinga – Tuangoma – Kigamboni

:km 61);

  • Middle Ring Road(Mbezi - Mbezi Mwisho – Kifuru – Banana – Kipara – Kigamboni : km 49);
  • ii.Daraja la Pili la Kigamboni (Magogoni – Kivukoni) ambapo maandalizi ya kufanya upembuzi yakinifu wa awali yanaendelea; na
  • iii.Barabara ya Himo – Moshi – Arusha (Tengeru – km 78).

Wizara inawakaribisha wawekezaji wenye nia kushiriki katika utekelezaji wa miradi hii na mingine itakayoibuliwa kwa ajili ya kutekelezwa kwa njia ya ubia. Wizara imepanga kufanya mkutano mkubwa na wawekezaji kwa lengo la kutangaza na kujadiliana kuhusu namna bora ya kutekeleza miradi hii kwa utaratibu wa PPP. Mkutano huo umepangwa kufanyika mwezi Julai 2024. Waheshimiwa wabunge mnakaribishwa sana.

  • 55.Mheshimiwa Spika, kwa upande wa miradi ya vivuko, kuna fursa mbalimbali katika uendeshaji wa vivuko hususan katika eneo la Kigamboni – Kivukoni. Kwa sasa, eneo la Kigamboni lina wakazi zaidi ya 300,000 ambapo wanaotumia usafiri wa kivuko ni wastani wa watu 60,000 kwa siku. Hata hivyo, kuna changamoto ya uchakavu wa vivuko vinavyohudumia katika eneo hilo, ambapo kwa sasa kivuko cha MV. Kazi pekee ndiyo kinafanya kazi kwa uhakika. Kivuko cha MV. Magogoni kinaendelea kufanyiwa ukarabati mkubwa. Kivuko cha MV. Kigamboni pia kipo katika matayarisho ya kufanyiwa ukarabati mkubwa. Hivyo, Serikali imeamua kushirikiana na Sekta Binafsi katika utoaji wa huduma za vivuko katika eneo hilo. Kwa sasa, TEMESA inashirikiana na Azam Marine Company Ltd kwenye utoaji wa huduma kivukoni hapo.

Wizara inaendelea kuangalia utaratibu bora zaidi wa ushirikiano huo ili kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na tija kwa pande zote mbili. Matarajio ya Wizara ni kuwa ushiriki wa sekta binafsi katika utoaji huduma za vivuko katika eneo la Kigamboni utaondoa kero kwa wananchi wanaotumia huduma hiyo.

Nitoe wito kwa wawekezaji wengine wenye nia kushirikiana na TEMESA katika utoaji wa huduma za vivuko katika maeneo mengine nchini. Aidha, tunawakaribisha wawekezaji kuingia ubia (Joint Venture) na TEMESA katika matengenezo ya magari na ukodishaji wa mitambo.

  • 56.Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kukemea taarifa za kupotosha zinazotolewa na vyombo vya habari kuhusu vivuko vya Kigamboni na kuzua taharuki kwa wananchi wa eneo hilo. Serikali ipo kazini na haiwezi kuhatarisha usalama wa raia wake kwa namna yoyote ile. Hivyo, niwaombe wananchi wa Kigamboni kuwa watulivu wakati Serikali inaendelea kuboresha huduma za vivuko pale Kigamboni, sambamba na maboresho ya barabara ya Kibada – Mwasonga Jct na Songani Jct – Kijata Jct yanayolenga kuifanya Kigamboni kuwa mji bora.
  • 57.Mheshimiwa Spika,kuhusumiradi ya nyumba,

TBA ina jumla ya nyumba na majengo 7,116 Tanzania Bara. Licha ya uwepo wa nyumba hizi, bado uhitaji wa


nyumba kwa watumishi wa umma (hata waheshimiwa wabunge) hapa Dodoma na wananchi wengine ni mkubwa ambapo inakadiriwa mahitaji halisi ni takriban nyumba milioni 3 nchi nzima. Katika kuongeza kasi ya uwekezaji katika nyumba, TBA imeweka mikakati mbalimbali ya kuongeza vyanzo vya fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi yake, ikiwa pamoja na kuboresha ushirikiano na sekta binafsi katika uendelezaji wa milki nchini.

Nitoe wito kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa, taasisi za kifedha, na wadau wa maendeleo kuchangamkia fursa hizi adhimu zilizopo katika sekta ya ujenzi ili pande zote mbili, yaani Serikali na wawekezaji binafsi wafaidike.

Matumizi ya Teknolojia Mpya

  • 58.Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TANROADS itaendelea kufanya tafiti mbalimbali katika kubaini teknolojia mpya, nafuu na zenye tijakatikamiradiya ujenzi. Maelezo ya kina kuhusu teknolojia hizo yameoneshwa katika Aya ya 224 225 ya Kitabu cha Hotuba ya Bajeti ya Wizara.

Udhibiti wa Ubora wa Barabara

  • 59.Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto ya kuharibika kwa barabara kabla ya muda wake, Wizara imepanga kuanza kutumia mitambo maalum ya kupima ubora wa barabara (Road Scanners). Matumizi ya teknolojia hii yatatuwezesha kupima ubora wa barabara kama X– ray inavyopima mwili wa binadamu. Wizara imeamua kutumia teknolojia hii ya kisasa ili kuondoa kabisa matumizi ya vifaa visivyostahili katika upimaji wa ubora wa barabara vinavyotumika kwa sasa. Hivyo sururu sasa basi. Matumizi ya mitambo hii yatadhibiti makandarasi wasio waaminifu wanaocheza na viwango vya ubora wa barabara wanazojenga. Mitambo iliyonunuliwa ina thamani ya Shilingi bilioni 5.1. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kununua mitambo hii. Ushirikishwaji wa Makundi Maalum katika Kazi za Barabara
  • 60.Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kutekeleza mikakati ya kuwajengea uwezo makundi maalum hususan wanawake na vijana ili kuongeza ushiriki wao katika kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara nchini. Katika mwaka wa fedha 2024/25, Wizara kupitia ERB, CRB na AQRB itaandaa mpango mahsusi wa kuwajengea uwezo

vijana kwa nyenzo na ujuzi ili waanzishe kampuni za ujenzi na ushauri elekezi zitakazoshiriki katika ujenzi wa miundombinu. Wizara ina mpango unaofanana na BBT kiuhandisi, ambao utawajengea vijana kesho iliyo bora kwa kutenga miradi ambayo itawaongezea uzoefu katika kazi zao.

  • 61.MheshimiwaSpika,mikakati mingine inayotekelezwa na Wizara ni pamoja na kuendesha programu ya SEAP na EAPP kupitia ERB na AQRB mtawalia. Programu hizi zinalenga kuwapatia ujuzi na uzoefu wahandisi wahitimu pamoja na wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ili waweze kusajiliwa kama wataalam (professionals). Vilevile, Wizara kupitia ICoT inaendesha mafunzo ya muda mrefu katika fani za ujenzi, umeme na mitambo katika ngazi za Astashahada na Stashahada ili kuzalisha wataalam watakaohudumia Sekta ya Ujenzi. Mafundi hawa ni muhimu sana katika utekelezaji wa kazi za ujenzi.

Vilevile ICoT inaendesha mafunzo maalum ya muda mfupi kwa makundi maalum ya vijana, wanawake, wazee na wasiojiweza ili kuwajengea uwezo wa kushiriki katika kazi za matengenezo ya barabara zinazotolewanaTANROADS na TARURA. Lengo la mafunzoyotenikuongezaushiriki wa makundi hayo muhimu katika shughuli za ujenzi wa


barabara. Wahitimu wa mafunzo haya huweza kuunda kandarasi kupitia CRB na hivyo kukidhi vigezo vya kupatiwa kazi za matengenezo ya barabara.

Nitoe rai kwa makundi ya vijana na wanawake kurasimisha na kuingiza sokoni kazi zao ili kuchangamkia fursa hii adhimu inayotolewa na Wizara. Wizara inaahidi kuwasimamia kwa kuzingatia taaluma zenu na kuwalea hadi kuwa kampuni kubwa zenye uwezo wa kushindana katika soko.


F. SHUKRANI

  • 62.Mheshimiwa Spika, kupitia hadhira hii, naomba kuwatambua na kuwashukuru Washirika mbalimbali wa Maendeleo pamoja na wadau wote ambao wameshirikiana nasi kwa namna moja au nyingine katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Wizara. Kipekee nawashukuru wafuatao: Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Dunia (WB), Japan (JICA), OPEC Fund, Korea Kusini (KOICA), Abu Dhabi Fund, Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU), Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB), Kuwait Fund, Barrick, EACOP, Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sekretarieti ya Jumuiya ya Nchi za SADC, Japan, China,Norway, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na PSSSF, Taasisi za fedha za CRDB, NMB, NBC na TCB na Asasi mbalimbali zisizokuwa za Serikali; Sekta Binafsi pamoja na wadau wengine wengi. Nawashukuru wadau hawa kipekee kwa kukubali kwa kauli moja kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa mkakati wa kuongeza ushiriki wa wazawa katika miradi ya ujenzi. Niseme tu kwamba asanteni sana.
  • 63.Mheshimiwa Spika, naomba nitoe tena shukrani zangu za dhati kwako na kwa Waheshimiwa Wabunge wote kwa kunisikiliza. Hotuba hii inapatikana pia katika tovuti ya Wizara (www.mow.go.tz).

G.MUHTASARI WA MAOMBI YA FEDHA YA WIZARA YA UJENZI KATIKA MWAKA WA FEDHA 2024/25

  • 64.Mheshimiwa Spika, fedha ninazoziomba pamoja na masuala mengine zitatumika kutekeleza kazi zifuatazo;
  • i.Kukamilisha miradi ya barabara 12 ambayo utekelezaji wake umefikia asilimia 70 au zaidi kama inavyooneshwa katika Aya ya 17 ya Kitabu cha Hotuba yangu;
  • ii.Kuendelea na miradi ya ujenzi wa barabara na madaraja 62 ambayo utekelezaji wake upo chini ya asilimia 70 lakini kazi zinaendelea (Aya ya 17 ya Kitabu cha Hotuba); na
  • iii.Kutekeleza miradi ya majengo ya Serikali, vivuko, karakana na viwanja vya ndege.
  • 65.Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/25, Wizara ya Ujenziinaombakuidhinishiwajumla ya Shilingi Trilioni moja, Bilioni mia saba sitini na tisa, Milioni mia mbili tisini na sita, Mia moja hamsini na mbili elfu (1,769,296,152,000.00)kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi Bilioni themanini na moja, Milioni mia nne na saba, Mia nne thelathini na nane elfu (81,407,438,000.00) ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida

ya Wizara na Taasisi na ShilingiTrilionimoja,Bilioni mia sita themanini na saba, Milioni mia nane themanini na nane, Mia saba kumi na nne elfu (1,687,888,714,000.00) kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

Kati ya fedha za Matumizi ya Kawaida, Shilingi Bilioni sabini na sita, Milioni mia tano themanini na nane, Mia mbili thelathini na tatu elfu (76,588,233,000.00) ni za Mishahara ya Watumishi na Shilingi Bilioni nne, Milioni mia nane kumi na tisa, Mia mbili na tano elfu (4,819,205,000.00) ni za Matumizi Mengineyo.

Bajeti ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inajumuisha fedha za ndani Shilingi Trilioni moja, Bilioni mia moja arobaini na moja, Milioni mia nane na tatu, Mia tisa themanini na tisa elfu (1,141,803,989,000.00) na fedha za nje ni Shilingi Bilioni mia tano arobaini nasita, Milioni themanini na nne, Mia saba ishirini na tano elfu (546,084,725,000.00). Fedha za ndani zinajumuisha Shilingi Bilioni mia tano tisini na tisa, Milioni mia saba hamsini na sita, Mia nne sitini na saba elfu na mia nane (599,756,467,800.00) kutoka Mfuko wa Barabara na Shilingi Bilioni mia tano arobaini na mbili, Milioni arobaini na saba, Mia tano ishirini na moja elfu na mia mbili (542,047,521,200.00) ni fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali.


  • 66.Mheshimiwa Spika, pamoja na Hotuba hii, nimeambatisha mchanganuo wa miradi itakayotekelezwa na Wizara katika mwaka wa fedha 2024/25 (Kiambatisho Na. 1 5). Naomba viambatisho hivyo vichukuliwe kama sehemu ya vielelezo vya hoja yangu.
  • 67.Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.