Maadili ya Msingi

TEMESA itafafanuliwa kwa maadili yafuatayo ambayo kila mtumishi atayasimamia na kuonyesha;


(i) Uadilifu: TEMESA inasimamia uaminifu kwa watumishi wake na uaminifu baina ya watumishi, wateja wa TEMESA, serikali na viongozi wa serikali ya Tanzania, wadau wengine wote na kwa kila mtu na kila shirika. Hawakubali au kutoa zawadi au hongo za thamani yoyote.


(ii) Kazi ya Ushirikiano: TEMESA inasimamia watumishi na kutambua kuegemea kwao na majukumu ya pamoja ya kuuwezesha Wakala kufanya kazi na kutimiza majukumu yake. Wanasifiwa kwa kushirikiana, kufanya kazi kwa pamoja na kuheshimiana ili kufikia malengo.


(iii) Utaalamu: TEMESA itahakikisha inachukua njia ambazo zinaonyesha udhibitishaji katika umahiri, tabia, mtazamo na mwenendo.


(iv) Uwajibikaji: TEMESA itahakikisha inawajibika kwa wadau wake na kwa taifa katika kutekeleza majukumu na jukumu lililopewa mamlaka.


(v) Uwazi: TEMESA itahakikisha uwazi katika shughuli zake zote na kuwa tayari kwa kupimwa na kuwajibika. Ili kufanikisha hili, Wakala utahakikisha kuwa kuna uwazi wa kifedha na usio wa kifedha na wa hiari kwa shughuli zake zote.