MRADI WA USIMIKAJI WA TAA ZA BARABARA BRT II, KUKUZA UJUZI WA MAFUNDI TEMESA

Meneja TEMESAKikosi cha Umeme, Mhandisi Pongeza Semakuwa amesema mradi wa usimikaji wa taa za barabarani kwa Barabara za mabasi yaendayo haraka/mwendokasi (BRT phase II) baina ya TEMESA na kampuni ya SINO HYDRO kutoka nchini China umewapa ujuzi na kuwajengea uzoefu mafundi wa TEMESA.