​UKARABATI MKUBWA MV. MAGOGONI WAFIKIA HATUA NZURI

Ukarabati mkubwa wa kivuko MV. MAGOGONI unaoendelea Mombasa Nchini Kenya umefikia hatua nzuri, ukarabati huo mkubwa unaojumuisha ununuzi na uwekaji wa mitambo yote mipya ya uendeshaji wa kivuko zikiwemo injini mpya na mitambo yake, uwekaji wa mabati mapya ya kivuko pamoja na vifaa vyote vya uongozaji wa kivuko, unafanywa na kampuni ya African Marine iliyoko eneo la Tangana, Mbaraki Mombasa Nchini Kenya.