MONGELLA AITAKA TEMESA KUCHANGAMKIA FURSA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella ameutaka Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kuchangamkia fursa za matengenezo ya magari ya Serikali na binafsi Mkoani humo. Mhe Mongella ametoa kauli hiyo leo Tarehe 24 Machi, 2023 wakati alipohudhuria kikao cha wadau wanaotumia huduma za Wakala huo Mkoani Arusha kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.