TEMESA YAWAPATIA MAMENEJA WAGAVI NA WAHASIBU MAFUNZO MFUMO WA MADENI
Mkurugenzi wa Huduma Saidizi Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) Bi. Josephine Matiro leo amefungua mafunzo kwa wahasibu, wagavi pamoja na Mameneja wa Mikoa. Mafunzo hayo ya siku moja yamefanyika katika ofisi za Makao Makuu ya Wakala huo yaliyopo maeneo ya Tambukareli mjini Dodoma na yamejikita katika ajenda mbili, ambayo ya kwanza nikuingiza madeni kwenye mfumo wa madeni wa TEMESA pili ni kuwafundisha mfumo wa manunuzi (Purchase Module).