SERIKALI YATOA BILIONI 17.8 UJENZI WA VIVUKO VIPYA VITATU MWANZA

Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni 17 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vivuko vipya vitatu Mkoani Mwanza. Vivuko hivyo vitatu, vimeanza kujengwa kwa ajili ya kutumika katika ziwa Victoria katika maeneo ya Ijinga Kahangala Wilayani Magu Mkoani Mwanza, Bwiro Bukondo Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza, pamoja na Nyakaliro Kome Halmashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.