NDUHIYE AIPONGEZA SERIKALI KWA KUTEKELEZA MPANGO WA MAFUNZO YA WATUMISHI WA VIVUKO TEMESA
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Bwana Ludovick Nduhiye ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) ulio chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa kuona umuhimu wa kutenga fedha katika bajeti yake kwa ajili ya kuwapatia mafunzo muhimu Watumishi wa Vivuko kote nchini.