KILAHALA NA TIMU YAKE WAZURU MTWARA
Lazaro Kilahala, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) pamoja na timu yake, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi (DBSS) Bi. Josephine Matiro pamoja na Mkurugenzi wa Matengenezo na Huduma za Ufundi (DMTS) Mhandisi. Hassan Karonda, leo wameendelea na ziara ya kiutendaji Mkoani Mtwara ambapo wametembelea karakana ya Mkoa huo na kuzungumza na watumishi, wamekagua utendaji kazi wa kivuko cha MV. MAFANIKIO kinachotoa huduma kati ya Msangamkuu na Msemo Mtwara Mjini kabla ya kuhitimisha ziara yao katika kivuko cha MV. KILAMBO kilichokuwa kinatoa huduma kati ya Kilambo Mtwara na Namoto Msumbiji. Kivuko hicho kimesimama kutoa huduma kwa muda mrefu kutokana na kukauka mara kwa mara kwa Mto Ruvuma na kusababisha kivuko kisimame kutoa huduma na kwa mujibu wa Kilahala, kivuko hicho kitafanyiwa ukarabati mkubwa na kuhamishwa kwenda kutoa huduma eneo jingine lenye uhitaji.