​MTENDAJI MKUU TEMESA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MKOA GEITA

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania Lazaro N. Kilahala leo amemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Reuben Shigella na kufanya nae mazungumzo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa iliyoko mjini Geita. Katika ziara hiyo ya kiutendaji, Mtendaji Mkuu ameambatana na mwenyeji wake Meneja wa Mkoa wa Geita Mhandisi Mahangaiko Ngoroma, Mkurugenzi wa Matengenezo na Huduma za Ufundi Mhandisi Hassan Karonda pamoja na Mkurugenzi wa Huduma Saidizi Bi. Josephine Matiro.