UKARABATI KIVUKO CHA MV. TANGA WAFIKIA HATUA NZURI

Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme nchini TEMESA inaendelea na utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa vivuko nchini ambavyo muda wake wa kukarabatiwa umefika ili viendeelee kutoa huduma vikiwa katika hali ya usalama, katika muendelezo huo, kivuko cha MV TANGA kinachotoa huduma kati ya Pangani na Bweni Wilayani Pangani Mkoani Tanga ni miongoni mwa vivuko ambavyo vinaendelea kufanyiwa ukarabati mkubwa