BALOZI AISHA ATEMBELEA OFISI ZA TEMESA MAGOGONI, AFURAHISHWA NA UTOAJI HUDUMA KWENYE KIVUKO
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) Balozi Aisha Amour, leo amefanya ziara ya kutembelea na kukagua huduma zinazotolewa katika kivuko cha Magogoni Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na kukagua, pia amesikiliza maoni ya wananchi kuhusu huduma zitolewazo katika kivuko hicho.