KATIBU MKUU UJENZI AITAKA TEMESA KUBORESHA HUDUMA ZAKE NA KULINDA MAPATO
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Balozi Mhandisi Aisha S. Amour leo amefanya kikao na menejimenti na mameneja wa Mikoa na vituo vya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) na kuwataka watumishi wa Wakala huo kuwajibika katika kutimiza majukumu yao ya kila siku kwa ufanisi na kulinda mapato. Katibu Mkuu amezungumza hayo leo wakati wa kikao kilichofanyika katika ukumbi wa VETA Dodoma ambapo amewaagiza mameneja wa Mikoa na vituo kuhakikisha wanaboresha mazingira ya kazi katika vituo vyao, wanalinda vyanzo vya mapato na kutumia fedha za Serikali kwa uwazi huku wakihakikisha kila mtumishi anawajibika katika majukumu yake ya kila siku.