MTENDAJI MKUU AHITIMISHA ZIARA YAKE KWA KUIPONGEZA KARAKANA YA VINGUNGUTI

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Lazaro Kilahala leo amehitimisha ziara yake ya siku mbili kwa kutembelea karakana za MT. Depot pamoja na karakana ya Vingunguti zilizopo jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na yote, amewapongeza watumishi wa karakana ya Vingunguti kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye karakana hiyo na kuifanya kuwa karakana ya mfano.