‘’TUANZE KUZIFANYIA KAZI CHANGAMOTO’’ MTENDAJI MKUU TEMESA
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Lazaro N. Kilahala leo amefanya ziara fupi ya kiutendaji na kuwaagiza watumishi wa Mkoa wa Dodoma kuanza kuyafanyia kazi malalamiko ya wateja wanaohudumiwa na karakana hiyo. Akiwa katika ziara hiyo fupi, Mtendaji Mkuu alianza kwa kutembelea karakana ya TEMESA Mkoa wa Dodoma, ametembelea pia eneo la ujenzi wa karakana mpya ya mfano inayojengwa eneo la Kizota pamoja na kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya la Makao Makuu ya Wakala huo linalojengwa katika eneo la NCC mtaa wa Tambukareli mjini Dodoma.