LAZARO N. KILAHALA MTENDAJI MKUU MPYA TEMESA
Lazaro N. Kilahala leo amekabidhiwa rasmi ofisi kutoka kwa Kaimu Mtendaji Mkuu aliyekuwa akishikilia ofisi hiyo kwa muda, Mkurugenzi wa Uendeshaji Bi. Monica A. Moshi. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za makao makuu ya Wakala wa Ufundi na Umeme zilizopo mjini Dodoma na kushuhudiwa na viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ambao walimuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.