MILIONI 400 ZANG'ARISHA BARABARA USHETU
Wakala wa Ufundi na Umeme nchini TEMESA kupitia Kikosi chake cha Umeme (Corporation Sole) umesimika taa za kumulika mitaa barabarani (street lights) zipatazo 100 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, takribani kilometa 52 kutoka Wilayani Kahama mjini Shinyanga. Taa hizo zilizogharimu takribani shilingi milioni 400 za Kitanzania zimesimikwa katika barabara ya kuelekea Wilaya ya Kahama katika Kijiji cha Mitonga kitongoji cha Mitonga A na Nyamilangano na zimekava eneo la kilometa takribani tatu.