ULEGA AUNDA TIMU KUCHUNGUZA KIVUKO CHA MV TANGA

Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega ameunda timu ya wataalamu na kuipa siku saba kuchunguza changamoto zinazojitokeza mara kwa mara katika Kivuko cha MV TANGA kilichopo wilayani Pangani, mkoani Tanga, baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kuhusu kusuasua kwa utendaji wake.